Wednesday, September 26, 2012

IET Week - Dodoma 2012



MAADHIMISHO YA WIKI YA WAHANDISI TANZANIA – DODOMA.
       (Motto: Uhandisi Kwa Maendeleo Ya Taifa)

Mh. Dr. Rehema Nchimbi Mkuu wa mkoa wa Dodoma akihutubia.
Maadhimisho yalifunguliwa na Mheshimiwa mkuu wa mkoa wa Dodoma Dr. Rehema Nchimbi. Katika Hotuba yake Dr. Rehema Nchimbi alizungumzia umuhimu wa kazi za kihandisi kutambulika na kuheshimika katika jamii yetu ya Tanzania na kwamba Maendeleo ya Nchi yeyote Duniani huletwa na wahandisi. Aliwaomba watanzania wasibeze kazi kubwa na nzuri zinazofanywa na wahandisi hapa nchini kwetu akitoa mifano ya Majengo makubwa (magorofa) na Barabara nyingi na madaraja makubwa hapa Dodoma  na Tanzania kwa ujumla ambazo zote zinajengwa kwa kiwango cha Lami, alisema ni kazi kubwa  inayofanywa na wahandisi.

Mheshimiwa aliwaomba Wahandisi watumie taaluma yao walionayo ya uhandisi katika kurekebisha Maadili ya Watoto na Vijana wa Tanzania ambayo kwa kiasi kikubwa sana yamemomonyoka .Aliendelea kwa kusisitiza mtandao wa internet na utandawazi ambapo sasa karibia kila mwananchi anaweza kuutumia umechangia kwa kiasi kikubwa katika mmomonyoko wa maadili kwa vijana wetu.Alisema “kwa nini msitengeneze software (najua kuna software Engineers) mvizuie hukohuko angani kabla havijawafikia watoto wetu?...najua mkiamua mnaweza hebu fanyeni kitu hali ni mbaya”

Hali Kadhalika Mheshimiwa aliwasifia wahandisi kwa kuaandaa maadhimisho haya ambayo ndo yamefanyika kwa mara ya kwanza mjini Dodoma na kuwa sio wachoyo kwa kuwaelimisha  wananchi wa Dodoma pindi wanapotembelea maonesho mbalimbali  kwani kufanya hivyo kunawaondolea wananchi hofu na kulaumu kusiko kwa lazima.Mfano alisema “Wananchi wamekuwa na Fikra potofu kuwa  Wahandisi wanajenga madaraja usiku tu…wahandisi ni wachawi” au “Hii barabara imejengwa ovyo yaani lami imewekwa chini halafu kokoto zinamwagwa juu……kumbe kuna maelezo ya kitaalamu hapo yanoyoweza kuwaondolea wananchi wasiwasi”. Aliwasihi wananchi wa Dodoma watembelee maonesho hayo yanayofanyika kwa wiki nzima ili waulize maswali yao na watajibiwa na wataalamu katika mabanda mbali mbali yaliopo viwanja vya Nyerere Square katikati kabisa ya mji wa Dodoma.


Pamoja na maonyesho hayo wahandisi wamejipanga kushiriki kikamilifu katika huduma mbalimbali za kijamii katika wiki hii ikiwa ni pamoja na Kwenda katika shule za msingi na sekondari zilizoko Dodoma mjini kufundisha masomo ya sayansi na kuwahamasisha wanafunzi wapende masomo ya sayansi na fani ya Uhandisi kwa ujumla.Vile vile watashiriki katika kufanya usafi wa mazingira maeneo ya Soko la Majengo Dodoma na kushiriki katika katika Malumbano makubwa ya Hoja (Debate)  yatakayofanyika katika shule ya City High School siku ya Ijumaa saa 2.30 hadi saa 4,(Maada isemayo: Science Subjects are Better than Art Subject.)

Ufunguzi huo Uliambatana na Burudani mbalimbali ambapo kikundi cha ngoma Asilia cha  “Hiari Ya Moyo” kilitumbuiza na kukonga nyoyo za watu walioohudhuria ufunguzi huo.

Eng. Dr. M. Mzee na Eng. Musa Semwenda wakifuatilia kwa makini burudani kabambe ya ngoma asilia kutoka kwa kikundi cha “Hiyari Ya Moyo” Dodoma.



Mh. Dr. Rehema Nchimbi akitembelea banda la TANROADS-Dodoma, Eng. Adelphina wa TANROADS akitoa maelezo ya miradi mbalimbali ya barabara mkoani Dodoma.Vile vile Mheshimiwa mkuu wa mkoa alitoa sifa kede kede kwa TANROADS jinsi walivyojipanga kuhakikisha barabara zote mjini hapa zinajengwa kwa kiwango cha Lami.









1 comment: